MOHAMMED-ALIHi leo nawaza, nawazua maswala tata

Huzuni menijaza, maiaji ovyo yalowapata

Wakaazi kuwaliza, vilio na huzuni yakata

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

Makala ya jicho pevu, yanayofanya kwa makini

Zaonyesha ulegevu, kwa usalama nchini

Serikali ni nyamavu, wakenya wamo taabani

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

Wana-adamu na hawa, wamegeuka hayawani

Ule upendo na usawa, umegeuka chuki yakini

Ile Amani ya kawa, mepotea tumo vitani

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

Mauaji kule Lamu, sisahau na Mpeketoni

Yalomwagika yote damu,sababu siasa na dini

Manduguna binamu, waangamia hamna Amani

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

Arobaini na saba wote, wanafunzi wa Garissa

Hadi leo twalia sote, utulivu mioyoni kukosa

Za kijasusi habari zote, mlipuuza kwa nini hasa

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

Baada ya upekuzi, upelelezi wa kina

Mwafanya ipi kazi, ama kazi kuhongana

Ya jicho pevu upekuzi,nauliza una maana?

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

Tambueni tumechoka, kwa habari za tanzia

Kila tunapoamka, ajali uhalifu yaua twalia

Zote twaweza epuka, iwapo mtabadili tabia

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

Tamati meshafika, ila kuandika sitachoka

Iwapo tungewajibika, kila mtu bila kuchoka

Tungeweza kuepuka, vifo na kilio liyotughubika

Serikali yafanyani? Wakenya waangamia

 

News Reporter
My name is Emmanuel Yegon. Trained Communicator, Passionate storyteller with a bias toward smartphone storytelling. I am the Co-Founder and Communications Director at Mobile Journalism Africa. This platform is dedicated for human interest stories and features. Ask me about #MoJo