Asubuhi tuamkapo

Mchana tuzungukapo

Na usiku tulalapo

Twajiuliza ni vipi?

 

Jana ilienda wapi?

Kesho mejificha wapi?

Leo tunaishi vipi?

Twajiuliza ni vipi?

 

Kuzaliwa salmini

Kuishi kwa Imani

Kifo na huzuni

Twajiuliza ni vipi?

 

Duniani mabilioni

Hewa safi mapafuni

Yatutosha sote aushini

Twajiuliza ni vipi?

 

Maisha kama maua

Furaha ndo kuchanua

Kunyauka ndo kuua

Twajiuliza ni vipi?

 

 

 

Wazee na wachanga

Wote wenda kwa mchanga

Rutuba kwa mimea kuchanga

Twajiuliza ni vipi?

 

Nini sababu ya maisha

Tambua kabla kuisha

Shugli zote kusitisha

Twajiuliza ni vipi?

Kifo ni nini hasa?

Kuhuzunisha kukwasa

Eti dhawabu ya anasa

Twajiuliza ni vipi?

 

Tajiri wabobea

Masikini kulemea

Wote kaburi lategea

Twajiuliza ni vipi?

 

Wema wafa mapema

Wabaya waishi vyema

Roho zote zalazwa pema

Twajiuliza ni vipi?

 

Ulimi mdogo kama ufa

Ila yaweza bomoa taifa

Yatoa laana na sifa

Twajiuliza ni vipi?

 

 

Wadhambi wakuu duniani

Mkombozi katoka mbinguni

Kwa niaba yetu kufa msalabani

Twajiuliza ni vipi?

 

Tulianguka dhambini

Wokovu hatukudhamini

Ila tuliupata kwa damu mtini

Twajiuliza ni vipi?

Hatufahamu ya mbinguni

Ila twaishi kwa tumaini

Twaogopa ya kuzimuni

Twajiuliza ni vipi?

 

Mema ni ya mbinguni

Mabaya ya kuzimuni

Yote metenda bado ya hukumuni

Twajiuliza ni vipi?

 

 

Kila siku twajiandaa

Mbinguni sote kupaa

Ila twajua hatujafaa

Twajiuliza ni vipi?

 

Tambua leo basi

Kuwa bado kuna nafasi

Wa mbingu na kuzimu farasi

Zangoja utende mema ama uasi

 

Mungu yupo kikweli

Ibilisi pia yupo ukifeli

Ndiye mkuu wa utapeli

Mwabudu mungu anastahili

 

 

News Reporter
My name is Emmanuel Yegon. Trained Communicator, Passionate storyteller with a bias toward smartphone storytelling. I am the Co-Founder and Communications Director at Mobile Journalism Africa. This platform is dedicated for human interest stories and features. Ask me about #MoJo