Bado Kitambo Kidogo

”Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.- (Ufunuo 22:12-13)

Yuaja!

Ajira anao mkononi

Kwa wale wanaomwamini

Wanaomwabudu kwa roho na kweli

Wenye kustahimili kila hali

Washindao majaribu kwa imani

Wote watakua naye uzimani

 

Msife moyo!

Yatendeni yaliyo mema

Kila siku muwe wenye mienendo mema

Mkikosea ombeni msamaha

Mkikosewa pia mjifunze kusamehe

Kwa vyovyote wasaidieni wasojiweza

Kwa wote muwe vielelezo,mwangaza

 

Inukeni, angazeni!

Watangazie wote upendo

Utamaduni wa nyumbani upendo

Wajuze wote neno lake

Waite waje zizini pake

Wafanye wote wawe wanafunzi

Wamjie baba mungu mwenyezi

 

Yesu yuaja tena!

Mmejiandaa vipi kumpokea?

Mtakua wapi siku atakapotokea

Mawinguni kuja kuikomboa kanisa?

Jiandaeni leo,jiandaeni sasa

Msije Mkaachwa siku hiyo

Tumlaki bwana sote atakapokuja siku hiyo.

 

Bado kitambo Kidogo

 

Bado Kitambo Kidogo.png

News Reporter
My name is Emmanuel Yegon. Trained Communicator, Passionate storyteller with a bias toward smartphone storytelling. I am the Co-Founder and Communications Director at Mobile Journalism Africa. This platform is dedicated for human interest stories and features. Ask me about #MoJo