Tafakari

Ubinadamu na utu

Wema mekosa kwa kila mtu

Mioyo watu mejaza kutu

Heri wanyama wa mwitu

 

Serikali mejaa wezi

Mashamba kuiba kila mwezi

Fedha kufuja ndio kazi

Ya vijana, walemavu na wazazi

 

Kuishi jiji kuu

Kweli utayaona makuu

Utapeli wa hali ya juu

Ama kweli ni mji mkuu

 

Askari wa baraza la jiji

Kuwahangaisha wauzaji

Watoa hukumu bila majaji

Eti wapate hongo-hitaji

 

Jiji megeuka shamba la wanyama

Sipostahimili talazimika kuhama

vurugu kila wakati hamna usalama

maovu mekua kawaida tazama

 

Taarifa zote mejaa utata

Viongozi kukicha wapigana vita

Meharibu dhana ya wakati wa Kenyatta

Kuwa Kenya hakuna matata

 

Ulimwengu umechanganyikiwa

Maovu yaendelea kusifiwa

Watu wema wadhulumiwa

Wengi bila hatia ovyo wauawa

 

Twahitaji badiliko la tabia

Tenda wema sipatikane na hatia

Kikosea omba msamaha pia

Tupendane, tuheshimiane pia

News Reporter
My name is Emmanuel Yegon. Trained Communicator, Passionate storyteller with a bias toward smartphone storytelling. I am the Co-Founder and Communications Director at Mobile Journalism Africa. This platform is dedicated for human interest stories and features. Ask me about #MoJo