Saratani Sio Gonjwa Wastani

 

Kansa au saratani

Gonjwa liwatishao wengi ulimwenguni

Jinamizi kuu lilozuka duniani

Litoka wapi gonjwa hili?

 

Gonjwa la rika zote

Halibagui jinsia laathiri zote

Halibagui kabila latuathiri sote

Litoka wapi gonjwa hili?

 

Mewageuza wengi mayatima

Yaua watoto,wazazi,jamii nzima

Mewaacha wengi kushika tama

Litoka wapi gonjwa hili?

 

Ila tusikate tamaa

Twaweza epuka balaa

Iwapo tutafanya inavyofaa

Tutaepuka gonjwa hili

 

Uvutaji wa sigara

Unywaji pombe kila mara

Vyote vyanzo vya madhara

Epuka uwe salama

 

Badili tabia na mienendo

Wingi wa matunda katika mlo ndio mtindo

Mazoezi kila mara uvivu kando

Uwe buheri wa siha

 

Tembelea vituo vya afya

Kila wakati uchunguzwe upya

Ikijulikana mapema itadhibitiwa

Uchunguzi wa saratani ni bure

 

Tushirikiane tuhamazishe jamii

Kuhusu athari za ugonjwa huu

Dalili na njia za kuudhibiti

Pamoja tuelimishane kama jamii

 

Saratani si utani

Mewauwa wengi mtaani

Ila tumechoka, sasa tumo vitani

Paza sauti za hamazisho nchini

Watu wapate kufahamu saratani

Sio gonjwa wastani

Fika leo hospitalini

Ufanyiwe uchunguzi

#PamojaTutashinda

#WeCancervive

 

Ungana nasi tarehe 4 mwezi huu katika kuhamazisha jamii kuhusu mbinu za kuudhibiti ugonjwa huu. Matembezi hayo yatafanyika mjini Eldoret. Usikose!C3KekiBVUAEAQkL.jpg

 

 

 

 

News Reporter
My name is Emmanuel Yegon. Trained Communicator, Passionate storyteller with a bias toward smartphone storytelling. I am the Co-Founder and Communications Director at Mobile Journalism Africa. This platform is dedicated for human interest stories and features. Ask me about #MoJo